Wednesday, 11 November 2015

Marekani yaahidi zawadi kwa habari kuhusu al-Shabab

 Al-Shabab

Marekani imeahidi $6 milioni kwa habari kuhusu aliko kiongozi wa al-Shabab
 
Marekani imehaidi kutoa zawadi ya jumla ya $27 milioni kwa yeyote atakayetoa habari zitakazowezesha kukamatwa kwa viongozi sita wakuu wa kundi la al-Shabab.
Wizara ya mashauri ya kigeni ya Marekani imetangaza kuwa Marekani itatoa $6 milioni kwa habari kumhusu Abu Ubaidah (Direye), $5 milioni kwa habari kuhusu kila mmoja kati ya Mahad Karate, Ma’alim Daud, na Hassan Afgooye, na $3 milioni kwa habari za kila mmoja kati ya Maalim Salman na Ahmed Iman Ali.
Viongozi hao wa kundi hilo la Somalia wanasakwa kwa kupanga mashambulio ya kigaidi likiwemo shambulio la Chuo Kikuu cha Garissa kaskazini mashariki mwa Kenya mwezi Aprili.
Marekani imesema sita hao wamekuwa wakihusika katika kufadhili, kusajili wanachama na kutoa mafunzo kwa wapiganaji wa al-Shabaab.
Bw Ubaidah alifanywa kiongozi wa al-Shabaab mwaka jana baada ya mtangulizi wake Ahmed Godane kuuawa kwenye shambulio la ndege za Marekani.
Ubaidah amesisitiza kwamba kundi hilo bado ni tiifu kwa Al Qaeda, ingawa majuzi kuna kundi la wapiganaji hao lililojiunga na Islamic State

No comments:

Post a Comment