Monday, 9 November 2015

MAONYESHO YA KIMATAIFA YA UTALII YAFANA SANA JIJINI MONTREAL, CANADA

Maonyesho ya 27 ya Kimataifa ya Utalii ambayo yamedumu kwa siku tatu mfululizo katika jiji la Montreal nchini Canada yafana sana. Ubalozi wa Tanzania, Ottawa nchini Canada ulikuwa ni mmoja wa washiriki kati ya washiriki waonyeshaji 400 walioalikwa na sekta ya utalii ambayo ndiyo muandaaji rasmi wa maonesho hayo.

Maonyesho hayo ambayo yamefanyika katika mahali maarufu  la “la Place Bonaventure” katika jiji la hilo, ambalo liko upande wa Mashariki mwa Canada, eneo ambalo wengi wa wakazi wake huzungumza Kifaransa, yamekuwa na hamasa na mashiko makubwa mwaka huu kwa kupata wahudhuriaji zaidi ya elfu thelathini na tatu (33,000).

Kutokana na wingi wa watu, wakiwemo watalii wanaopenda kuzuru nchi mbalimbali, waliohamasika kuhudhuria maonesho hayo, Balozi wa Tanzania Mhe. Jack Mugendi Zoka aliamua kuwa kati ya waonyeshaji na watoa taarifa za vivutio vya utalii katika banda lake kama ionekanavyo katika picha hapo chini.

Aidha, mabalozi wa nchi mbalimbali walifika katika banda la utalii la Tanzania kujionea ni jinsi gani limeweza kuwa kivutio cha watalii wengi. Balozi wa nchi jirani ya Kenya alikuwa miongoni mwa watembeleaji katika banda hilo.

No comments:

Post a Comment