Wednesday, 22 June 2016

Hatima ya Umoja wa Ulaya inafungamanishwa na matokeo ya kura ya maoni ya Uingereza



Rais Francois Hollande wa Ufaransa anasema mustakbali wa Ulaya unategemea matokeo ya kura ya maoni ya Uingereza kama itasalia au itatoka katika Umoja wa ulaya. Rais Hollande amesema hayo baada ya mazungumzo pamoja na waziri mkuu wa Slovakia Robert Fico, mnamo mkesha wa kura ya maoni ambapo Waingereza watachagua kama wanataka nchi yao itoke au Brexit au isalie katika Umoja wa ulaya. Rais Hollande anasema Paris itauangalia uamuzi wa waingereza kuwa "usiobadilishika" na kuongeza "London itakumbwa na hatari kubwa ikiwa haitokuwa na njia ya kuingia katika soko la pamoja. Rais Francois Hollande wa Ufaransa alikuwa kila mara akiitetea umuhimu wa Uingereza kusalia katika Umoja wa Ulaya. Wito kama huo umetolewa pia na kansela Angela Merkel wa Ujerumani hii leo. "Bila ya shaka ninataka Uingereza iendelee kuwa mwanachama wa Umoja wa ulaya lakini uamuzi wanao wananchi wa Uingereza" amesema Kansela Merkel mbele ya maripota baada ya mazungumzo pamoja na Waziri Mkuu wa Poland, Beata Szydlo

No comments:

Post a Comment