Monday, 9 May 2016



Wamachinga kukamatwa

Na Hamidu Abdallah

Dar es salaam

Halmashauri ya manispaa ya Ilala inatarajia kupitisha msako wa kuwakamata na kuwafikisha mahakamani  wafanya biashara wadogo wadogo  maarufu kama Wamachinga watakaokiuka agizo walilopewa na halmashauri hiyo.

Halmashauri hiyo imetoa agizo kwa kwa wafanyabiashara hao kuondoka na kuacha kufanya biashara zao katika viunga vyote vya jiji na kwenda katika maeneo waliyopangiwa ili kuacaha utamaduni wa kufanya biashara barabarani kwa kuepusha misangamano na kuacha jiji safi.

Hayo yalibainika Mwishoni mwa wiki iliyopita katika ukumbi wa halmashauri hiyo ambapo Mkurugenzi wa halmashauri ya Ilala Isaya Mngurumi alipokuwa akiongea na waandishi wa habari juu ya agizo hilo.

“Tumewapa siku tatu yaani kuanzia leo ijumaa waje kwa afisa mipango miji wea halmashauri ili waelekezwe pakwenda na mwisho  jumaapili ikifika jumaatatu tunaanza msako wa kuwakamata watakao kaidi”, alisema Mkurugenzi  Mngurumi.

Mkurugenzi Mngurumi alibainisha kuwa Jumla ya masoko mannne yenye uwezo wa kuwaweka wafanyabiashara zaidi  ya 6000 yametengwa ambayo ni soko la Kigogo freshi lenye uwezo wa kuwa na wafanyabiashara 1500, soko la Tabata muslim uwezo wake wafanyabiashara 1166, soko la Kivule lenye uwezo wa kuwa na wafanya biashara 1000 na soko la Ukonga na lenye uwezo wa kuwa na wafanyabiashara 1500.

Na leo ndio jumaatatu ya zoezi kuanza ambapo msako huo utahusisha wafanyabiashara wasio n maduka maalum, wanaopanga kando kando mwa barabara za wapita kwa miguu na wale wanaopanga biashara zao katika barabara za mabasi yaendayo kasi maarufu kama DAT.

Msako huo utafanywa na kamati ya ulinzi na usalama wa halmashauri ya manispaa ya Ilala kwa kushirikiana na jeshi la polisi na mgambo wa jiji wa JKT hivyo wafanyabiashara hao wametakiwa kutii agizo bila ya shurti.

No comments:

Post a Comment