Wednesday, 18 May 2016

Licha ya kipigo cha goli 1-0 kutoka kwa GD Esperanca, Yanga imetinga hatua ya Makundi Kombe la CAF

Siku 11 baada ya klabu ya Dar es Salaam Young Africans kucheza mchezo wake wa kwanza wa hatua ya mtoano ya 16 ya Kombe la shirikisho barani Afrika CAF, Leo May 18 2016 Yanga waliifuata GD Esperanca ya Angola kucheza mchezo wa marudiano, katika mchezo huo Yanga imekubali kipigo cha goli 1-0.
Goli ambalo lilifungwa na Kabungula dakika ya 25, kwa matokeo hayo Yanga wanafanikiwa kutinga hatua ya Makundi ya Kombe la shirikisho barani baada ya kuitoa Esperanca kwa jumla ya goli 2-1, hiyo inatokana na Yanga kuifunga Esperanca goli 2-0 katika mchezo wa kwanza uliochezwa uwanja wa Taifa Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment