Wednesday, 25 May 2016

Watanzania 8 waliotaka kujiunga na al-Shabab wakamatwa

Serikali ya Kenya imefichua kwamba imewakamata raia wanane wa Tanzania waliokuwa katika harakati za kujiunga na kundi la wapiganaji la al-Shabab nchini Somalia.

Katika taarifa iliotumwa katika vyombo vya habari, polisi wanasema raia hao waliokamatwa katika kipindi cha miezi miwili iliopita walikiri kuwa mbioni kujiunga na kundi hilo la ugaidi.
Hatua hiyo inajiri siku chache baada ya kundi la watu wanaojidai kuwa wapiganaji wa Kiislamu kuweka video mtandaoni likidai uwepo wa wapiganaji wa Kiislamu nchini Tanzania
Video hiyo iliwaonyesha wanaume hao wakiwa wamejifunika nyuso zao kwa vitambaa na barakoa.
Wanadai wamo katika mji wa Tanga na kuwahimiza Waislamu katika taifa hilo la Afrika Mashariki kujiunga na kampeni yao
Polisi wa Kenya pia wanasema wamefanikiwa kutibua njama ya wanachama wa kundi linalojiita Islamic State ya kutekeleza mashambulio nchini humo na kuwakamata washukiwa wawili.
Wawili hao Kiguzo Mwangolo Mgutu na Abubakar Jillo Mohammed walipewa mafunzo ya kuwa na itikadi kali kabla ya kuingizwa katika kundi la IS na Mohammed Ali aliyekamatwa awali na ambaye anasaidia polisi na uchunguzi, polisi wamesema.
Kulingana na taarifa hiyo, kufuatia kukamatwa kwa Mohammed Ali, wafuasi wake wamekuwa wakipanga kufanya mashambulizi ya kulipiza kisasi sana wakilenga sekta ya uchukuzi wa abiria.
Kukamatwa kwa wawili hao, kumezuia kutokea kwa mashambulio katika miji ya Nairobi na Mombasa.

RAIS DKT.MAGUFULI AMTEUA ALIYEKUWA WAZIRI MKUU, MIZENGO PINDA KUWA MKUU WA CHUO KIKUU HURIA.

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgo9cAS1gRPxzxJpVaYZ1i4Af7kmcFxXLuNFrObJaS-pCCLjygYML0r0KOGxj3Fu4I2lfEGMJ4_mbm1ojH2ezwDVUfR3gxEK_NcRB3ePsbt_snt6AVCzxF-gmy6-U5Vmc1SWcPVdBCGhV0/s1600/53a40a13-51a2-49f2-8f6d-990d1d524dd3.jpg

Wednesday, 18 May 2016

UWANJA WA NDEGE MWANZA UJENGWE KISASA ILI KUINUA SEKTA YA UTALII.

Na Tiganya Vincent-MAELEZO, Dodoma.
BAADHI ya Wabunge wanaotoka Kanda ya Ziwa wameomba Wizara ya Ujenzi , Uchukuzi na Mawasiliano kujenga Uwanja wa Ndege wa Mwanza kwa kiwango cha Kimataifa ili kuimarisha sekta ya Utalii na usafiri wa anga katika kanda ya Ziwa. Walisema kuwa hatua itasaidia watalii wanaokuja nchini kushuka moja kwa moja mkoani Mwanza na kisha kuelekea katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na maeneo mengine ya vivutio vya hapa nchini bila kupitia nchi jirani.
Kauli hiyo imetolewa jana na Wabunge Dkt.Raphael Chegeni  na Mhe. Ezekeil Maige wakati wakichangia hotuba kuhusu utekelezaji wa bajeti ya Wizara ya Ujenzi ,Uchukuzi  na Mawasiliano kwa mwaka ujao wa fedha.
Mhe. Dkt.Chegeni alisema kuwa Uwanja wa Ndege wa Mwanza ni muhimu ukajengwa kwa viwango vya Kimataifa ili uweze kuruhusu ndege mbalimbali kubwa na ndogo kuweza kutua bila tatizo.
Alisema kuwa hatua hiyo itasaidia kuunganisha Mkoa wa Mwanza na nchi jirani za Rwanda, Uganda na Burundi na hivyo kuruhusu ndege nyingi kutoka Nchi hizo kutua bila kwenda katika Uwanja wa Mwalimu Julius Nyerere.
Mhe. Dkt. Chegeni  aliongeza kuwa uwanja huo endapo utajengwa kwa kiwango cha Kimataifa utasaidia kuwa kiungo muhimu kwa mikoa 10 ya kanda ya ziwanana kati.
Naye Mbunge wa Jimbo la Msalala Mhe. Maige alisema kuwa ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Mwanza sio tu utasaidia kuunganisha mkoa huo na mikoa mingine bali utasaidia kuchochea  uchumi wa eneo la Kanda ya Ziwa na Tanzania kwa ujumla kwani watalii na wasafiri wengine watakuwa na fursa ya kuingia Mwanza bila kupitia nchi jirani.
Aliongeza kuwa endapo zoezi hilo litafanyika kwa kiwango cha kimataifa litatoa fursa kwa ndege nyingi za ukumbwa tofauti tofauti kutua katika Uwanja huo na hivyo kupunguzia wananchi ughali wa bei unaotozwa na baadhi ya Kampuni za Ndege ambazo zinatoa huduma za usafiri mkoani humo.

VYANZO VYA MAPATO VYA SERIKALI VIANGALIWE UPYA –CAG

 Naibu  Katibu Mkuu Menejimenti ya utumishi wa Umma na Utawala Bora , Susan Mlay akizungumza na wajumbe wa baraza la wafanyakazi wa ofisi ya CAG leo jijini Dar es Salaam.
 Mdhibiti Mkuu wa hesabu za Serikali, CAG Profesa Mussa Assad akizungumza na waandishi wafanyakazi ofisi hiyo wakati mkutano baraza jpya la wafanyakazi la wafanyakazi iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
 Naibu  Katibu Mkuu Menejimenti ya utumishi wa Umma na Utawala Bora , Susan Mlay akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa baraza la wafanyakazi wa ofisi ya CAG leo jijini Dar es Salaam.

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
OFISI ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za serikali imeitaka serikali kuangalia upya vyanzo vyake vya mapato na matumizi ya fedha  kwa sasa sio nzuri.

Akizungumza katika mkutano wa kwanza wa Baraza jipya la wafanyakazi wa ofisi hiyo, Mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za Serikali, CAG Profesa Mussa Assad hiyo ni changamoto ambayo inapaswa kuangaliwa na kutafutiwa ufumbuzi na changamoto zinazoikabili ofisi yake, amesema kuchelewa kupokea mgao wa fedha za miradi ya maendeleo kwa wakati inasababisha ofisi hiyo kushindwa kutekeleza mipango na kukamilisha miradi husika kwa wakati.

Profesa Assaad amesema  idadi ya watumishi iliyokuwepo katika ofisi yake ilikuwa 81 ikaongezeka hadi kufika 150 lakini bado wanahitaji watumishi wengine 129 wenye fani ya ukaguzi.

Aidha amesema  kuwa kulingana na weledi wa wakaguzi hao Tanzania imeteuliwa kukaimu nafasi ya uenyekiti wa Bodi ya Ukaguzi ya Umoja wa Mataifa nafasi ambayo ilikuwa ikishikiliwa na China iliyomaliza muda wake mwaka 2014.

Nae Naibu  Katibu Mkuu Menejimenti ya utumishi wa Umma na Utawala Bora , Susan mlay amesema watumishi wanatakiwa kuwa na weledi katika kufanya kazi ili kuleta tija kwa taifa ikiwa pamoja na kuangalia masilahi yetu kutokana na kazi wanazozifanya.

TFDA YAWA MWENYEJI WA MAFUNZO YA WADAU KUHUSU USALAMA WA CHAKULA BARANI AFRIKA



Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) imekuwa mwenyeji wa mafunzo ya siku tano, tarehe 16 – 20 Mei, 2016, kwa wadau wa udhibiti katika mnyororo wa Usalama wa Chakula hususan upimaji katika maabara Barani Afrika.
Akifungua mafunzo hayo yaliyowashirikisha wadau wapatao 50 kutoka nchi 15 za Afrika, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Mpoki Ulisubisya, alisema kuwa Lengo kuu la mafunzo na mkutano ni kujadili majukumu, wajibu na mchango wa kila mdau katika suala zima la kuhakikisha chakula ni salama kwa walaji.

Dr. Mpoki alisema, “ni matumaini yangu kuwa mafunzo haya yataongeza uelewa wa namna bora ya usimamizi wa mifumo ya udhibiti wa Chakula Salama kwa kubadilishana uzoefu miongoni mwa wadau mliopo hapa’ .
Naye Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Bw. Hiiti Sillo, wakati wa kutoa maelezo ya awali kuhusu mafunzo hayo yanayodhaminiwa na Taasisi ya Kimataifa ya Nguvu za mionzi (IAEA), alieleza kuwa kufanyika kwa mafunzo haya nchini Tanzania ni heshima kubwa na ishara ya mwendelezo wa TFDA kufikia Dira yake ya kuwa taasisi inayoongoza barani Afrika katika kudhibiti usalama, ubora na ufanisi wa chakula, dawa, vipodozi na vifaa Tiba.

Nchi zinazoshiriki katika mafunzo haya ni pamoja na Algeria, Benin, Botswana, Cameroon, Egypt, Ethiopia, Mauritius, Mali, Chadi, Namibia, Sudan, Tunisia, Uganda, Zimbabwe na Tanzania. Matokeo ya mafunzo haya yatakuwa ni dira ya utekelezaji wa mradi wa udhibiti wa mnyororo wa Usalama wa Chakula kabla ya kufikia mwisho wa mwezi Disemba 2016.

Wadau wa mnyororo wa udhibiti wa Usalama wa Chakula walioshiriki katika mafunzo haya wanatoka kwenye maeneo ya maabara, ukaguzi, uzalishaji wa vyakula na walaji.

Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Bw. Hiiti Sillo, akitoa maelezo ya awali katika ufunguzi wa mafunzo kwa washiriki wa Kongamano kuhusu Usalama wa Chakula kwa wadau kutoka nchi 11 za Bara la Afrika. 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Mpoki Ulisubisya (aliyekaa katikati), akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa Mafunzo ya siku tano kuhusu Usalama wa Chakula kwa wadau kutoka nchi 11 za Afrika. Wengine waliokaa ni Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Bw. Hiiti Sillo, Mkurugenzi wa Huduma za Maabara wa TFDA, Bi. Charys Ugullum, Mwakilishi wa FAO na Mwakilishi wa IAEA, Bw. Alex Mulori.

KATIBU MKUU WA UCHUKUZI AFANYA ZIARA YA KUSTUKIZA KATIKA MTAMBO WA KUPIMA MAFUTA (FLOW METER) BANDARI YA DAR ES SALAAM

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

KATIBU Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano –Uchukuzi, Mhandisi Dk. Leonard Chamuriho amesema kuwa kasoro ambazo zimejitokeza katika mtambo wa kupima mafuta Bandarini (Flow Meter) zinapatiwa ufumbuzi na mkandasi wa vifaa vya mitambo hiyo.

Akizungumza leo na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Chamuriho amesema kuwa mtambo huo lazima uangaliwe kwa umakini kutokana na serikali ndipo inapata kodi yake halisi ya mafuta yanayoshuwa na meli.

Amesema kuwa mkandarasi msambazaji vifaa kutokana na mkataba ni lazima ahakikishe kwa vitu viliyopata kasoro kutatua kabla ya tatizo halijawa kubwa au kutojirudia.

Aidha amesema kuwa suala la kamera ambazo zimepata hitilafu baada ya kupigwa na radi zitengenezwe mara moja na tatizo lisijirudie wakati mwingine kutokana na umhimu wa kamera katika eneo hilo.

Amesema kutokana hali hiyo amemtaka Kaimu Meneja wa Bandari kupeleka taarifa jumatatu ikiwa na ina vitu vyote ambavyo vipo katika mradi wa mtambo huo.
Kwa upande wa Meneja Mradi Mtambo wa kupima mafuta, Mhandisi Mary Mhayaya amesema kuwa jana kumetokea changamoto katika mtambo iliyotokana na mafuta kukwama kutokana na uchafu ambapo wameweza kusafisha.
Aidha amesema katika majaribio wa mtambo huo umeweza kuwa na mafanikio baada ya meli tatu kushusha mafuta bila matatizo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano –Uchukuzi, Mhandisi Dk. Leonard Chamuriho akipata maelekezo kutoka kwa Meneja Mradi wa Mtambo wa Kupima Mafuta wa TPA, Mhandisi Mary Mhayaya leo wakati ziara kushtukiza na katibu Mkuu huyo Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano –Uchukuzi, Mhandisi Dk. Leonard Chamuriho akiwa juu ya mtambo akiangalia miundombinu yake wakati wa ziara ya kushtukiza katika mtambo wa kupima mafuta Kigamboni, jijini Dar es Salaam.

WATUHUMIWA WA UBAKAJI WAFIKISHWA KORTIN NA KUSOMEWA MASHITAKA YAO

Watuhumiwa wa Ubakaji Huko Dakawa,Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro wakipelekwa Kortini Mjini humo kusomewa Mashtaka yao mapema leo.


Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Morogoro imewapandisha kizimbani washtakiwa sita wakikabiliwa na mashtaka matatu tofauti, wakiwemo washtakiwa wawili wanaokabiliwa na mashtaka na kubaka na kumuingilia kinyume na maumbile bila ridhaa yake binti mwenye umri wa miaka 21 mkazi wa Wami Dakawa Wilayani Mvomero.

Katika kesi hiyo iliyovuta hisia ya mamia ya wananchi wa mkoa wa Morogoro, washtakiwa Iddi Adam Mabena (21) mkazi wa Njombe na Zuberi Thabit (30) mkazi wa Mbarali Mbeya wamefikishwa mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi  wa Mahakama ya mkoa wa Morogoro Mary Moyo, wakikabiliwa na shtaka la kubaka na kulawiti, wanalodaiwa kutenda aprili 27 mwaka huu majira ya usiku katika nyumba ya kulala wageni ya Titii iliyopo Wami Dakawa wilayani Mvomero.

Upande wa Serikali katika shtaka hilo lililofanyika faragha kwa mujibu wa sheria, umewakilishwa na waendesha mashtaka Gloria Rwakibalila, Edgar Bantulaki na Calistus Kapinga. Washtakiwa wote wawili wamekana mashtaka na kesi hiyo imepangwa kufikishwa tena Juni Mosi mwaka huu  kwa ajili ya kutajwa.
Upande wa mashtaka umewasilisha kiapo cha pingamizi la dhamana kwa ajili ya usalama wa washtakiwa kwa vile shauri hilo limegusa hisia ya jamii na kwa  vile upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika, hivyo washtakiwa wanaweza kuharibu upelelezi.
Katika shtaka jingine lililofikishwa mbele ya Hakimu Ivan Msaki wa Mahakama hiyo, washtakiwa sita wakiwemo Iddi Mabena, Zuberi Thabiti na wengine wanne Rajab Salehe, Ramadhani Ally Makunja anayetetewa na wakili Ignas Punge, Muhsin Ngai na John Petter maarufu kama Paroko, wakazi wa Wami Dakawa wilayani Mvomero wanadaiwa kusambaza picha chafu na za ngono kwa njia ya mtandao kinyume na sheria ya makosa ya mtandao no 14 ya mwaka 2015.

Washtakiwa wote sita wamekana mashtaka ambapo upande wa mashtaka ukiongozwa na mawakili watatu wa serikali uliomba washtakiwa wanyimwe dhamana kwa usalama wao na kutoharibu upelelezi kwa vile bado haujakamilika, huku ule wa mshtakiwa namba nne ukiomba kuwasilisha kiapo cha kupinga mshtakiwa kunyimwa dhamana, ambapo suala hilo la dhamana katika shauri hilo litafikishwa tena juni mosi kwaajili ya kujadiliwa na washtakiwa wote wamerudishwa rumande.

Licha ya kipigo cha goli 1-0 kutoka kwa GD Esperanca, Yanga imetinga hatua ya Makundi Kombe la CAF

Siku 11 baada ya klabu ya Dar es Salaam Young Africans kucheza mchezo wake wa kwanza wa hatua ya mtoano ya 16 ya Kombe la shirikisho barani Afrika CAF, Leo May 18 2016 Yanga waliifuata GD Esperanca ya Angola kucheza mchezo wa marudiano, katika mchezo huo Yanga imekubali kipigo cha goli 1-0.
Goli ambalo lilifungwa na Kabungula dakika ya 25, kwa matokeo hayo Yanga wanafanikiwa kutinga hatua ya Makundi ya Kombe la shirikisho barani baada ya kuitoa Esperanca kwa jumla ya goli 2-1, hiyo inatokana na Yanga kuifunga Esperanca goli 2-0 katika mchezo wa kwanza uliochezwa uwanja wa Taifa Dar es Salaam
Mwanamke mmoja katika muungano wa milki za kiarabu amepigwa faini na kurudishwa kwao baada ya kupatikana akiingia katika faragha ya mumewe.
Vyombo vya habari vinasema kuwa mwanamke huyo alichukua na kufungua simu ya mumewe baada ya kumshuku kwamba alikuwa na uhusiano wa kando.
Mumewe alilalamika kwa maafisa wa polisi na mkewe akashtakiwa chini ya sheria ya uhalifu wa mtandaoni, kulingana na chombo cha habari cha Gulf News.
Mwanamke huyo ambaye jina lake lilibanwa na ambaye ni mgeni katika muungano wa milki za kiarabu alipigwa faini ya pauni 28,000.
Alikiri mahakamani kwamba aliifungua simu ya mumewe bila ya ruhusa na kuzituma picha katika simu yake wakili wake aliiambia Gulf News.
Wakili huyo Eman Sabt,alisema kwamba wanandoa hao walikuwa na umri wa miaka ya 30 na wenye asili ya kiarabu,lakini hakutoa maelezo zaidi

Sunday, 15 May 2016

Barcelona win La Liga: Real Madrid boss admits rivals deserved to win

Barcelona
Barcelona scored 24 goals without conceding once in their final five games
Real Madrid boss Zinedine Zidane conceded Barcelona are deserved La Liga champions after losing out to their arch-rivals by one point.
Real won their last 12 league games, but Barca ended with five victories in a row after a blip in April saw their lead over Real closed from 10 points.
"We're all disappointed, but with 38 matchdays played, we can't change anything now," said Zidane, who has won 21 of his 26 games in charge.
"Barcelona deserved to win La Liga."
Luis Enrique, who has won the title in both his seasons in charge of Barcelona, agreed with his rival.
"It was a deserved title which shows that the team knows how to bounce back from a bad spell.
"We played very well over the full season, we were on top of the table for many weeks and the most consistent team wins the title."
Captain Andres Iniesta has now won eight La Liga titles, a third of Barcelona's total league championships. Barca have won six of the last eight titles - including two in a row.
"La Liga is glorious," the Spain midfielder said. "It is the competition of stability, the one we are able to win year after year. Whenever you win the league, it is a great season."
Defender Gerard Pique said: "This is a historic time for the club. This is a unique generation of footballers with loads of talent and who are achieving things that have never been done before.
"We had a negative run that meant we had to fight right to the last, but we got our prize in the end."
Both sides have a cup final yet to play. Barca face Sevilla in next Sunday's Copa del Rey final, while Real face city rivals Atletico in the Champions League final on Saturday, 28 May
Bao lililofungwa na Danielle carter lilikisaidia kikosi cha wanawake wa timu ya Arsenal kuchukua taji la 14 la kombe la FA baada ya kutawala mechi dhidi ya Chelsea katika uwanja wa Wembley.
Carter,ambaye alipiga juu alipopata nafasi yake ya kwanza aliipatia the Gunners uongozi baada ya kuvamia lango la Chelsea.
Asisat Oshoal baadaye alikosa fursa tatu za wazi kuongeza ushindi huo wa Arsenal.
Fran Kirby alipoteza nafasi ya wazi ya kusawazisha kutoka upande wa Chelsea katika mechi ya fainali iliohudhuriwa na mashabiki 32,912.
Mshambuliaji huyo wa Uingereza alikosa mwelekeo katika kipindi cha kwanza na hivyobasi kumpatia fursa kipa sari Van Veenendaal kuokoa mikwaju yake.

Saturday, 14 May 2016

RAIS MAGUFULI AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA UWANJA WA NDEGE DAR ES SALAAM

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameiagiza Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi kwa kushirikiana na vyombo vya dola kuchukua hatua mara moja dhidi ya dosari za ukaguzi zilizopo katika kitengo cha ukaguzi wa mizigo na abiria katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (Terminal One) Dar es salaam.

Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo tarehe 13 Mei, 2016 alipofanya ziara ya kushtukiza katika uwanja huo na kubaini kuwa mashine za ukaguzi za sehemu ya kuwasili abiria na mizigo hazifanyi kazi kwa muda mrefu.

Maafisa wa uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere waliokuwa wakitoa maelezo juu ya hali ya kitengo cha ukaguzi wa mizigo na abiria katika uwanja huo, walikuwa wakitoa taarifa zinazotofautiana kuhusu utendaji kazi wa mashine za ukaguzi, hali iliyosababisha Dkt. Magufuli aamue kuiagiza wizara husika kwa kushirikiana na vyombo vya dola kuchukua hatua mara moja.
“Unajua mimi sipendi kudanganywa, ni vizuri uzungumze ukweli tu, kwa nini nimeanzia hapa huwezi ukajiuliza? eeeh sasa sipendi kudanganywa, ukinidanganya nitachukia sasa hivi, wewe umenidanganya kwamba hiyo ndio mbovu na hii ndio nzima, nikawaambia muiwashe hiyo nzima, akaja huyu mwenzako amezungumza ukweli kabisa, akasema hii ni mbovu kwa miezi miwili."Dkt. Magufuli aliwahoji Maafisa wa uwanja wa ndege
“Kwa hiyo mizigo inayoingia humu huwa hamuikagui kwa namna yoyote ile, kwa hiyo mtu nikiamua kuja na madawa yangu ya kulevya, nikaja na dhahabu zangu, na almasi zangu na meno ya tembo kwa kutumia hizi ndege ndogondogo napita tu” Rais Magufuli aliendelea kuwabana maafisa hao wa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere
Rais Dkt. John Pombe Magufuli amefanya ziara hii ya kushtukiza mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere akitokea Jijini Kampala nchini Uganda ambako jana alihudhuria sherehe ya kuapishwa kwa Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni

YANGA YAWAKUNA MASHABIKI WAKE,WAIBUKA NA KOMBE LA LIGI KUU MSIMU WA 2015/2016


KOMBE LATUA JANGWANI: Chereko na nderemo uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam wakati Waziri wa Kilimo Mwigulu Nchemba akiikabidhi Yanga Kombe la Ligi Kuu. Huu ni ubingwa wa 26.Yanga walikabidhiwa kombe hilo na Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Mh Mwigulu Nchemba, ambae ndie alikuwa mgeni rasmi.

TANZANIA KUSHIRIKIANA NA JUMUIYA YA MADOLA – MAJALIWA

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Jumuiya ya Madola inaweza kuiga mbinu ambazo Tanzania imetumia katika kupambana na rushwa zikiwemo za kujumuisha wadau tofauti kwenye vita hiyo.

Ametoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki wakati akizungumza na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola, Bibi Patricia Scotland walipokutana kwenye mkutano wa kimataifa uliojadili jinsi ya kupambana na rushwa duniani uliofanyika Lancaster House, jijini London, Uingereza.

“Tanzania iko tayari kushirikiana na ninyi katika kujenga timu hii na ili uweze kupata picha halisi, nakukaribisha Tanzania uje ujionee hatua ambazo tumechukua hadi kufikia hapa tulipo kwenye vita hii dhidi ya rushwa,” alisema Waziri Mkuu ambaye alihudhuria mkutano huo kwa niaba ya Rais Dk. John Pombe Magufuli.

Alimweleza Katibu Mkuu huyo kwamba Serikali ya Awamu ya Tano imefanikiwa kupambana na rushwa kutokana na ushirikiano mkubwa inaoupata kutoka kwa wananchi. “Wananchi wanafurahia juhudi za Serikali, vyama vya kiraia pia vinaunga mkono jitihada zetu na vyombo vya habari vinashirikiana nasi katika vita hii,” alisema.

Waziri Mkuu alitoa wito huo baada ya kuelezwa na Bibi Scotland kwamba anataka kuanzisha idara malum kwenye Jumuiya hiyo ambayo itasimamia mapambano dhidi ya rushwa na makosa ya jinai.

“Nataka tuwe na idara yenye watu mahiri wa idara za uhasibu, mahakama yenyewe ikiwemo waendesha mashtaka na wanasheria kutoka kwenye nchi kadhaa ili washirikishane uzoefu kutoka kwenye nchi zao. Ninaamini katika nchi 53 ambazo ni wanachama wetu, sitakosa watu wa aina hii,” alisema.

Alisema ameamua kufanya hivyo ili aweze kuendanana na malengo makuu matatu ya jumuiya hiyo ambayo ni kupiga vita rushwa, kuhimiza utawala bora na usimamizi wa demokrasia

WAZIRI MKUU MAJALIWA: MAPAMBANO YA RUSHWA YANAHITAJI JUHUDI ZA PAMOJA



WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema mkutano wa kimataifa uliojadili jinsi ya kupambana na rushwa duniani ni kiashiria tosha kwamba tatizo la rushwa ni kubwa sana na linataka juhudi za pamoja katika kukabiliana nalo. (It’s a serious graft that needs concerted efforts).
Ametoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki wakati akizungumza na Waziri wa Nchi wa Uingereza anayeshughulikia Maendeleo ya Kimataifa, Bibi Justine Greening walipokutana kwenye mkutano huo uliofanyika Lancaster House, jijini London, Uingereza.
Waziri Mkuu ambaye alihudhuria mkutano huo kwa niaba ya Rais Dk. John Pombe Magufuli, alimweleza Bibi Greening kwamba viongozi wa Serikali wa awamu ya tano wameamua kwa dhati kupambana na kila ovu linalotokana na janga la rushwa na pia wameamua kuwajibika na kuachana na tabia ya kufanya kazi kwa mazoea.
“Sasa hivi nchi yetu ina utamaduni mpya wa kufanya kazi na tumeamua kufanya kazi kwelikweli na siyo tena kwa mazoea, tumeamua kuweka utamaduni mpya wa kupiga vita rushwa ili kuleta uwajibikaji na uwazi miongozi mwa watu wetu,” alisema.
Alipoulizwa ni kitu kimechangia kufanya Tanzania ing’are kimataifa katika vita hii, Waziri Mkuu alijibu kwamba Tanzania imetumia mambo manne ambayo ni kuzuia rushwa isitolewe ama kupokelewa (prevention), kampeni za kuelimisha jamii, kufanya mapitio ya sheria na kuwepo kwa utashi wa kisiasa.
“Serikali inachukua hatua za kiutawala na kisheria kama vile kuanzisha mahakama maalum ya mafisadi ambayo inatarajiwa kuanza kazi mwezi Julai mwaka huu,” alisema Waziri Mkuu.
Kwa upande wake, Bibi Greening alipongeza hatua zinazochukuliwa na Serikali ya awamu ya tano katika kupambana na rushwa na kwamba ndiyo maana Tanzania ilipewa mwaliko maalum wa kushiriki mkutano huo kwa vile baadhi ya mataifa yanaziona juhudi zinazofanywa na Serikali.
Pia alitumia fursa hiyo kumpongeza Waziri Mkuu kwa nia ambayo Serikali ya awamu ya tano imeionyesha katika kuwa na mpango wa kuendeleza viwanda.
Pia alimhakikishia Waziri Mkuu kwamba nchi yake iko tayari kuisaidia Tanzania kwenye mpango wake ilionao wa kupeleka umeme vijijini (Rural Electrification Programe). “Tuko tayari kuwasiidia kutekeleza mpango huu kupitia taasisi ya Energy Africa Initiative ambayo inapata ufadhili kupitia Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Uingereza (DFID),” alisema.
Wakati huohuo, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anayeshughulikia masuala ya kimataifa, Bibi Sarah Sewall ameipongeza Tanzania kwa kupiga hatua katika mapambano dhidi ya rushwa na kusisitiza kwamba makampuni mengi ya Marekani yana nia ya kuja kuwekeza Tanzania.
“Ninaamini uwekezahji huu utasaidia kuleta maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa watu wetu. Tunampongeza Rais Dk. Magufuli kwa juhudi anazofanya na nipende kusisitiza kwamba ushirikiano baina ya Tanzania na Marekani utaendelezwa katika maeneo yetu ya siku zote,” alisema.
Waziri Mkuu alimshukuru Bibi Sewall na kumsisitiza asiache kusaidia kuwahimiza wamarekani wengi waje kutalii Tanzania na wawekezaji zaidi waje kuwekeza nchini katika nyanja mbalimbali zikiwemo uanzishaji wa viwanda, uongezaji thamani kwenye mazao yanayozalishwa nchini na kuhakiksha kuwa Watanzania wanajifunza teknolojia mpya na za kisasa.

Thursday, 12 May 2016

kufuatia mauwaji ya watu saba Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu atoa saa 24 kuwatia nguvuni wale wote waliohusika

Mhe. Makamu wa Rais leo ametembelea Wilaya ya Sengerema kata ya Sima ambapo usiku wa kuamkia jana kulifanyika mauwaji ya kinyama ya watu saba wa familia moja ya Mama na watoto zake kuuwawa kwa kukatwa mapanga na watu wasiojulikana.Mhe. Makamu wa Rais Mama Suluhu Hassan ametoa masaa 24 kwa uongozi wa mkoa wa Mwanza pamoja na jeshi la polisi na vyombo vingine kuwatia nguvuni wale watu wote waliohusika na mauaji hayo.
Pichani ni makaburi yakiandaliwa kwa ajili ya kuzikwa kwa miili saba ya familia moja mapema leo Wilayani Sengerema .
Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu akisalimiana na kuwapa pole ndugu jamaa na marafiki kufuatia mauaji hayo ya watu saba wilayani Sengerema
Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Bi Zainab Telack pamoja na Mkuu wa mkoa wa jiji la Mwanza Mh.John Mongella wakiwa na Mgeni wao Makamu wa Rais Mh.Samia Suluhu alipokewenda kutoa pole kwenye tukio la mauwaji ya kinyama ya watu saba wa familia moja ya Mama na watoto zake kuuwawa kwa kukatwa mapanga na watu wasiojulikana ndani ya wilaya hiyo katika kijiji cha Sima mkoani Mwanza .
Makamu wa Rais Mh Samia Sulluh akizungumza kwenye tukio la mauwaji ya kinyama ya watu saba wa familia moja ya Mama na watoto zake kuuwawa kwa kukatwa mapanga na watu wasiojulikana,ambapo Mh.Samia ametoa saa 24 kukamatwa kwa wale wote waliohusika na tukio hilo la Kinyama

mahakama yaiamuru Kampuni ya TIGO kuwalipa mwana FA na AY zaidi ya Bil. 2

Mahakama ya Hakimu Mkazi Ilala imeiamuru kampuni ya Mawasiliano ya TIGO kuwalipa wasanii Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' na Ambwene Yessaya 'AY' jumla ya shilingi bilioni 2.18.

Fedha hizo ni za fidia baada ya kutumia nyimbo yao kama Caller Tune(Mwitikio wa simu) bila ruhusa wala mkataba